Sala za Jioni za Kwaresma 2021 SWAHILI - Book - Page 9
Somo (Danieli 3:26-27, 29-30, 34, 42.)
Kiongozi:
Wote:
Ee Bwana nioshe kabisa kutokana na hatia yangu
na unisafishe kutokana na dhambi zangu.
Kushoto:
Sifa kwako, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu,
na unastahili sifa;
na jina lako ni tukufu milele!
Kulia:
Kazi zako zote ni za kweli
na njia zako zote sawa,
na hukumu zako zote ni za kweli.
Kushoto:
Tumefanya dhambi na tumevunja sheria yako
kwa kugeuka kutoka kwako.
Hatukutii amri zako,
hatujafanya yale uliyotuamuru
kwa faida zetu wenyewe.
Kulia:
Kwa jina lako usife moyo nasi milele,
wala usifute agano lako.
Usitutie aibu,
lakini tushughulikie katika uvumilivu wako
na kwa rehema zako nyingi.
Kushoto:
Utuokoe kulingana na kazi zako za ajabu,
na uliletee utukufu jina lako, Ee Bwana.
Wote:
Kwa Mtawala wa enzi, asiyekufa, asiyeonekana,
Mungu pekee mwenye hekima,
pewa heshima na utukufu, kupitia mwanao Yesu
Kristo, milele na milele. Amina.
Ee nioshe zaidi na zaidi kutokana na hatia yangu
na unitakase dhambi zangu.
Kwa Wiki ya Kwanza, endelea hapa chini
Kwa Wiki ya Pili, geukia uk 15
Kwa Wiki ya Tatu, geukia uk 20
Kwa Wiki ya Nne, geukia uk 25
Kwa Wiki ya Tano, geukia uk 30
Zaburi
9